Tenzi za Rohoni 82 – Sioni haya kwa Bwana

Tenzi za Rohoni 82 – Sioni haya kwa Bwana

Tenzi Na. 82

Soma maneno kamili ya Tenzi za Rohoni namba 82, “Sioni haya kwa Bwana”, kwa ajili ya ibada, kuimba na kujifunza.


Maneno ya Wimbo

Sioni haya kwa Bwana
Kwake nitang’ara!
Mti wake sitakana,
Ni neno imara!
Msalaba ndio asili ya mema,
Nikatua mzigo hapo;
Nina uzima, furaha daima,
Njoni kafurahini papo.
Kama kiti chake vivyo
Ni yake ahadi,
Alivyowekewa navyo
Kamwe havirudi.
Bwana wangu, tena Mungu
Ndilo lake jina!
Hataacha roho yangu
Wala kunikana.
Atakiri langu jina,
Mbele za Babaye,
Anipe pahali tena
Mbinguni nikae.


Tazama Tenzi za Rohoni 1–164


Omba App ya Tenzi za Rohoni kwa Android

banner
Scroll to Top