Tenzi za Rohoni 74 – Wachunga Walipolinda
Tenzi Na. 74
Soma maneno kamili ya Tenzi za Rohoni namba 74, “Wachunga Walipolinda”, kwa ajili ya ibada, kuimba na kujifunza.
Maneno ya Wimbo
Wachunga walipolinda
Kucha nyama zao,
Malaika mtukufu
Alishuka kwao.
Wakacha sana wachunga,
Akawatuliza,
“Nawaletea habari
Ya kuwapendeza.”
“Mji ule wa Daudi
Leo amezawa
Mwokozi ni Kristo Bwana,
Ilivyoandikwa”.
“Huyo mwana wa Mbinguni
Ataonekana,
Amelazwa kihorini
Malazi hapana.”
Alipokwisha yanena
Malaika hao
Waliimba wimbo huu
Usio na mwisho:
“Enzi ni yake Munju juu,
Na nchi salama,
Kwa watu nao radhi kuu,
Sasa na daima.”