Tenzi za Rohoni 55 – Nipe Moyo Wenye Sifa
Tenzi Na. 55
Soma maneno kamili ya Tenzi za Rohoni namba 55, “Nipe Moyo Wenye Sifa”, kwa ajili ya ibada, kuimba na kujifunza.
Maneno ya Wimbo
Nipe moyo wenye sifa
Sio wa utumwa;
Moyo ulionyunyizwa
Damu ya thamani.
Moyo msikizi, moyo
Wa kunyenyekea,
Moyo utawaliwao
Na Mwokozi pia.
Mwenye kutubu, mnyonge,
Sadiki, amini;
Kamwe, kamwe asitengwe
Akaaye ndani.
Mpya, mwema na mawazo
Mwingi wa mapenzi
Nawe uwe kielelezo
Moyo wa Mwokozi.
Ni uule moyo wako;
Moyo wa huruma
Yesu, natamani kwako
Kukujua vyema.
Na ya midomo matunda
Yako, nipe nami;
Amani isiyokoma
Iwe yangu mimi.
Nitie yako tabia,
Inishukie juu;
Jina lako nipe pia,
Ndilo la upendo.
Ni wa baba utukufu;
Mwana atukuke;
Na roho Mtakatifu
U utatu pweke.