Tenzi za Rohoni 14 – Yesu kwa imani
Tenzi Na. 14
Soma maneno kamili ya Tenzi za Rohoni namba 14, “Yesu kwa imani”, kwa ajili ya ibada, kuimba na kujifunza.
Maneno ya Wimbo
Yesu kwa imani,
Nakutumaini,
Peke yako;
Nisikie sasa,
Na kunitakasa,
Ni wako kabisa
Tangu leo.
Nipe nguvu pia
Za kusaidia
Moyo wangu;
Ulikufa wewe,
Wokovu nipewe
Nakupenda wewe,
Bwana wangu.
Hapa nazunguka
Katika mashaka,
Na matata;
Palipo na giza
Utaniongoza
Hivi nitaweza
Kufuata.
Takuwa mzima
Nivushe salama
Mautini;
Sina hofu kamwe
Ukiwapo name
Nami nikwandame
Siku zote.