Tenzi za Rohoni 68 – Mungu Msaada Wetu

Tenzi za Rohoni 68 – Mungu Msaada Wetu

Tenzi Na. 68

Soma maneno kamili ya Tenzi za Rohoni namba 68, “Mungu Msaada Wetu”, kwa ajili ya ibada, kuimba na kujifunza.


Maneno ya Wimbo

Mungu msaada wetu
Tangu myaka yote,
Ndiwe tumaini letu
La zamani zote.
Kivuli cha kiti chako
Ndiyo ngome yetu.
Watosha mkono wako
Ni ulinzi wetu.
Kwanza havijakuwako
Nchi na milima,
Ndiwe Mungu; chini yako
Twakaa salama.
Na myaka elfu ni kama
Siku moja kwako;
Utanilinda daima
Tu wenyeji wako.
Binadamu huondoka,
Mwisho hana kitu;
Kama ndoto hutoweka
Ndivyo hali yetu.
Ila wewe Mungu wetu
Ndiwe wa kudumu;
Ndiwe bora, ngome yetu
Twakaa dawamu.


Tazama Tenzi za Rohoni 1–164


Omba App ya Tenzi za Rohoni kwa Android

banner
Scroll to Top