Tenzi za Rohoni 51 – Mungu Twatoa Shukrani
Tenzi Na. 51
Soma maneno kamili ya Tenzi za Rohoni namba 51, “Mungu Twatoa Shukrani”, kwa ajili ya ibada, kuimba na kujifunza.
Maneno ya Wimbo
Bwana Yesu atakuja, Vumilia!
Omba, ukiwa na haja, Vumilia!
Mbingunu Mungu aliko, Mwamini Mwokozi wako,
Nawe utafika huko, Vumilia!
Ikikucheka dunia, Vumilia!
Mwovu atakuvizia, Vumilia!
Hataweza kukushinda, Bwana Yesu akulinda,
Roho yako, akupenda, Vumilia!
Na ukiwa hatarini, Vumilia!
Dhiki nyingi duniani, Vumilia!
Vyatupasa kuyakuta, Majaribu na matata,
Na Bwana hakutuficha; Vumilia!
Adui wakikutana, Vumilia!
Na ndugu wakikukana, Vumilia!
Zote, zote zitakwisha, Nguvu zote za kutisha
Mungu chini atashusha; Vumilia!
Moyoni una majonzi, Vumilia!
Ndiyo bonde-ya-machozi, Vumilia!
Hima tutaandamana, Kwetu Mbinguni na Bwana
Tena hatutaachana; Vumilia!