Tenzi za Rohoni 30 – Nilikuwa kondoo aliyepotea

Tenzi za Rohoni 30 – Nilikuwa kondoo aliyepotea

Tenzi Na. 30

Soma maneno kamili ya Tenzi za Rohoni namba 30, “Nilikuwa kondoo aliyepotea”, kwa ajili ya ibada, kuimba na kujifunza.


Maneno ya Wimbo

Nilikuwa kondoo aliyepotea,
Sikupenda zizi kamwe, ila kutembea
Nilikuwa mwana asiyesikia,
Sikupenda baba yangu wala kutulia.
Na mchunga mwema alinitafuta,
Baba kwa mapenzi ndiye aliyenivuta;
Karibu ya kufa, kwa kiu na kwa njaa,
Waliniona mnyonge, waliniokoa.
Yesu ni mchunga, mwenziwe hapana,
Aliosha taka zangu, dhambi nyingi sana;
Kwa vidonda vyangu alitia dawa.
Ndiye aliyenipata, na kwake nalindwa.
Nilikuwa kondoo aliyepotea
Sasa nampenda Baba, na mchunga pia;
Kwanza nilitanga na kukosa sana,
Hivi nyumbani mwa Baba sipotei tena.


Tazama Tenzi za Rohoni 1–164


Omba App ya Tenzi za Rohoni kwa Android

banner
Scroll to Top