Tenzi za Rohoni 29 – Baba yetu aliye Mbinguni

Tenzi za Rohoni 29 – Baba yetu aliye Mbinguni

Tenzi Na. 29

Soma maneno kamili ya Tenzi za Rohoni namba 29, “Baba yetu aliye Mbinguni”, kwa ajili ya ibada, kuimba na kujifunza.


Maneno ya Wimbo

Baba yetu aliye Mbinguni
Amenifurahisha yakini
Kuniambia mwake chuoni
Ya kuwa nami Yesu pendoni.
Anipenda Mwokozi Yesu,
Anipenda, anipenda;
Anipenda Mwokozi Yesu,
Anipenda mimi.
Nimuachapo kutanga mbali,
Yeye yu vivyo, hupenda kweli,
Hunirejeza kwake moyoni;
Kweli yu nami Yesu pendoni.
Anipenda! Nami nampenda;
Kwa wokovu alionitenda;
Akanifia Msalabani
Kwa kuwa nami Yesu pendoni.
Haya kujua yanipa raha;
Kumuamini kuna furaha;
Humfukuza mara shetani,
Kwona yu nami Yesu Pendoni.
Sifa ni nyingi asifiwazo,
Moja ni sana katika hizo,
Wala siachi, hata Mbinguni,
Kwimba, “Yu nami Yesu pendoni”.


Tazama Tenzi za Rohoni 1–164


Omba App ya Tenzi za Rohoni kwa Android

banner
Scroll to Top