Tenzi za Rohoni 106 – Mungu Awe Nanyi Daima

Tenzi za Rohoni 106 – Mungu Awe Nanyi Daima

Tenzi Na. 106

Soma maneno kamili ya Tenzi za Rohoni namba 106, “Mungu Awe Nanyi Daima”, kwa ajili ya ibada, kuimba na kujifunza.


Maneno ya Wimbo

Mungu awe nanyi daima,
Hata twonane ya pili,
Awachunge kwa fadhili,
Mungu awe nanyi daima.
Hata twonane huko juu,
Hata twonane kwake kwema;
Hata twonane huko juu,
Mungu awe nanyi daima.
Mungu awe nanyi daima;
Ziwafunike mbawaze,
Awalishe, awakuze;
Mungu awe nanyi daima.
Mungu awe nanyi daima;
Kila wakati wa shani
Awalinde hifadhini;
Mungu awe nanyi daima.
Mungu awe nanyi daima;
Awabarikie sana,
Awapasulie kina;
Mungu awe nanyi daima.


Tazama Tenzi za Rohoni 1–164


Omba App ya Tenzi za Rohoni kwa Android

banner
Scroll to Top