Tenzi za Rohoni 106 – Mungu Awe Nanyi Daima
Tenzi Na. 106
Soma maneno kamili ya Tenzi za Rohoni namba 106, “Mungu Awe Nanyi Daima”, kwa ajili ya ibada, kuimba na kujifunza.
Maneno ya Wimbo
Mungu awe nanyi daima,
Hata twonane ya pili,
Awachunge kwa fadhili,
Mungu awe nanyi daima.
Hata twonane huko juu,
Hata twonane kwake kwema;
Hata twonane huko juu,
Mungu awe nanyi daima.
Mungu awe nanyi daima;
Ziwafunike mbawaze,
Awalishe, awakuze;
Mungu awe nanyi daima.
Mungu awe nanyi daima;
Kila wakati wa shani
Awalinde hifadhini;
Mungu awe nanyi daima.
Mungu awe nanyi daima;
Awabarikie sana,
Awapasulie kina;
Mungu awe nanyi daima.