Tenzi za Rohoni 100 – Tumrudie Bwana

Tenzi za Rohoni 100 – Tumrudie Bwana

Tenzi Na. 100

Soma maneno kamili ya Tenzi za Rohoni namba 100, “Tumrudie Bwana”, kwa ajili ya ibada, kuimba na kujifunza.


Maneno ya Wimbo

Mbona washangaa njiani?
Mbona warejea nyuma?
Warudi tena gizani
Alimokutoa Bwana?
Ni ya bure yote haya,
Uliyofunzwa ya Mungu?
Ni bure amekufia
Bwana Yesu kwa uchungu?
Wamtia kristo aibu
Na maneno yake pia?
Siku yaja ya hesabu,
Utamjibuje Bwana?
Upandapo tena hayo,
Halafu utayavuna.
Rudi kwa Bwana upesi,
Mwombe akupokee tena.


Tazama Tenzi za Rohoni 1–164


Omba App ya Tenzi za Rohoni kwa Android

banner
Scroll to Top