Tenzi za Rohoni 98 – Huyo Ndiye! Anashuka
Tenzi Na. 98
Soma maneno kamili ya Tenzi za Rohoni namba 98, “Huyo Ndiye! Anashuka”, kwa ajili ya ibada, kuimba na kujifunza.
Maneno ya Wimbo
Huyo ndiye! anaskuka,
Aliyetufilia,
Wengi waliookoka,
Wakimfurahia,
Aleluya!
Yesu aturudia.
Sote tutamtazama,
Amekaa kitini,
Nao waliomcoma,
Kumkaza mtini,
Na kilio, wamuone enzini.
Alama za kifo chake
Hata sasa anazo
Na waaminifu wake
Wapendezewa nazo.
Alipata,
Kwetu alama hizo.
Wokovu utakiwao
Sasa wapatikana,
Na watakatifu hao
Mbinguni wakutana
Kumlaki,
Ndiyo siku ya Bwana
Wakusujudie wote
Mbele ya kiti chako.
Zako, Bwana, nguvu zote
Itwae milki yako
Njoo Bwana,
Sisi tu watu wako.