Tenzi za Rohoni 70 – Yesu Atuchunga
Tenzi Na. 70
Soma maneno kamili ya Tenzi za Rohoni namba 70, “Yesu Atuchunga”, kwa ajili ya ibada, kuimba na kujifunza.
Maneno ya Wimbo
Yesu atuchunga,
Mchunga wetu,
Naye atufuta
Machozi yetu;
Mkononi mwake
Hatuna hofu,
Daima twapata
Kwake wokovu.
Yesu atuchunga
Tumemjua,
Na sauti yake
Twaitambua;
Naye akituonya
Ni kwa upole,
Tu kondoo zake
Hata milele.
Yesu atuchunga;
Aliwafia
Kondoo wakubwa
Na wana pia;
Kwamba awajua,
Kondoo zake,
Hutiwa alama
Ya damu yake.
Yesu atuchunga;
Mikono yake
Imewaambata
Kondoo zake;
Hapati wadhuru
Adui yule,
Yesu awalinda.