Tenzi za Rohoni 63 – Ndugu wa kirohoni
Tenzi Na. 63
Soma maneno kamili ya Tenzi za Rohoni namba 63, “Ndugu wa kirohoni”, kwa ajili ya ibada, kuimba na kujifunza.
Maneno ya Wimbo
Ndugu wa kirohoni
Mliokombolewa,
Tafakarini sana
Yatupasayo.
Wapenzi wake Yesu
Tuliokombolewa
Tujitoe kabisa
Wengi waponywe.
Siku itatimia
Tutakapoulizwa
Wale wa nyumba zetu
Na majirani
Tujitoeni, ndugu,
Tukahubiri Injili.
Atutumie Roho
kuponya wengi.
Wasiokombolewa
Ni wengi vijijini,
Wataokolewaje
Tukiogopa?
Bwana alijitoa
Akapotewa mengi,
Ili atuokoe,
Tusiwe waoga.
Aliyetununua,
Kwa kuimwaga damu,
Angalieni sana
Msimwepuke.