Tenzi za Rohoni 58 – Mwamba Wenye Imara

Tenzi za Rohoni 58 – Mwamba Wenye Imara

Tenzi Na. 58

Soma maneno kamili ya Tenzi za Rohoni namba 58, “Mwamba Wenye Imara”, kwa ajili ya ibada, kuimba na kujifunza.


Maneno ya Wimbo

Mwamba wenye imara
Kwako nitajificha!
Maji hayo na damu
Yaliyotoka humu,
Hunisafi na dhambi,
Hunifanya mshindi.
Kwa kazi zote pia ,
Sitimizi sharia.
Nijapofanya bidii,
Nikilia nakudhii,
Hayaishi makosa;
Ndiwe wa kuokoa.
Sina cha mkononi,
Naja Msalabani;
Nili tupu, nivike;
Ni mnyonge, nishike;
Nili mchafu naja,
Nioshe nisijafa.
Nikungojapo chini,
Nakwenda kaburini;
Nipaapo Mbinguni,
Na kukwona enzini:
Roho yangu na iwe
Rahani mwako wewe.


Tazama Tenzi za Rohoni 1–164


Omba App ya Tenzi za Rohoni kwa Android

banner
Scroll to Top