Tenzi za Rohoni 38 – Twende Kwa Yesu

Tenzi za Rohoni 38 – Twende Kwa Yesu

Tenzi Na. 38

Soma maneno kamili ya Tenzi za Rohoni namba 38, “Twende Kwa Yesu”, kwa ajili ya ibada, kuimba na kujifunza.


Maneno ya Wimbo

Twende kwa Yesu mimi nawe,
Njia atwonya tuijue
Imo Chuoni; na Mwenyewe,
Hapa asema, Njoo!
Na furaha tutaiona,
Mioyo ikitakata sana,
Kwako, Mwokozi, kuonana,
Na milele kukaa.
“Wana na waje”, atwambia,
Furahini mkisikia,
Ndiye mfalme wetu pia,
Na tumtii, Njoo.
Wangojeani? Leo yupo;
Sikiza sana asemapo;
Huruma zake zikiwapo,
Ewe kijana, Njoo.


Tazama Tenzi za Rohoni 1–164


Omba App ya Tenzi za Rohoni kwa Android

banner
Scroll to Top