Tenzi za Rohoni 25 – Nimekombolewa na Yesu

Tenzi za Rohoni 25 – Nimekombolewa na Yesu

Tenzi Na. 25

Soma maneno kamili ya Tenzi za Rohoni namba 25, “Nimekombolewa na Yesu”, kwa ajili ya ibada, kuimba na kujifunza.


Maneno ya Wimbo

Nimekombolewa na Yesu
Aliyenirehemia;
Kwa bei ya mauti yake
Nimekuwa mtoto wake.

Kombolewa!
Nakombolewa na damu;
Kombolewa!
Mimi mwana wake kweli.

Kukombolewa nafurahi,
Kupita lugha kutamka;
Kulionyesha pendo lake,
Nimekuwa mtoto wake.

Nitamwona uzuri wake,
Mfalme wangu wa ajabu;
Na sasa najifurahisha,
Katika neema yake.

Najua taji imewekwa
Mbinguni tayari kwangu;
Muda kitambo atakuja,
Ili alipo, niwepo.


Tazama Tenzi za Rohoni 1–164


Omba App ya Tenzi za Rohoni kwa Android

banner
Scroll to Top