Tenzi za Rohoni 17 – Namwadama Bwana
Tenzi Na. 17
Soma maneno kamili ya Tenzi za Rohoni namba 17, “Namwadama Bwana”, kwa ajili ya ibada, kuimba na kujifunza.
Maneno ya Wimbo
Namwadama Bwana kwa alilonena
Njia yangu huning’azia;
Nikimridhisha atanidumisha
Taamini nitii pia.
Amini utii, njia pweke ni hii
Ya furaha kwa Yesu: amini ukatii.
Giza sina kwangu wala hata wingu
Yeye mara huviondoa
Woga, wasiwasi, sononeko, basi;
Huamini nitii pia.
Masumbuko yote, sikitiko lote;
Kwa mapenzi hunilipia;
Baa, dhara, dhiki, vivyo hubariki
Taamini nitii pia.
Mimi sitajua raha sawasawa
Ila yote Yesu kumpa;
Napata fadhili na radhi kamili,
Taamini nitii pia.
Nitamfurahia na kumtumaini,
Majumbani na njia-njia;
Agizo natenda, nikitumwa hwenda,
Huamini nitii pia.