Tenzi za Rohoni 10 – Usinipite!
Tenzi Na. 10
Soma maneno kamili ya Tenzi za Rohoni namba 10, “Usinipite!”, kwa ajili ya ibada, kuimba na kujifunza.
Maneno ya Wimbo
Usinipite Mwokozi,
Unisikie;
Unapozuru wengine,
Usinipite.
Yesu,Yesu,
Unisikie;
Unapozuru wengine,
Usinipite.
Kiti chako cha rehema,
Nakitazama;
Magoti napiga pale,
Nisamehewe.
Sina ya kutegemea,
Ila Wewe tu;
Uso wako uwe kwangu;
Nakuabudu.
U Mfariji peke yako;
Sina Mbinguni,
Wala duniani pote,
Bwana mwingine.