Tenzi za Rohoni 7 – Ni Tabibu Wa Karibu

Tenzi za Rohoni 7 – Ni Tabibu Wa Karibu

Tenzi Na. 7

Soma maneno kamili ya Tenzi za Rohoni namba 7, “Ni Tabibu Wa Karibu”, kwa ajili ya ibada, kuimba na kujifunza.


Maneno ya Wimbo

Ni tabibu wa karibu;
Tabibu wa ajabu;
Na rehema za daima;
Ni dawa yake njema.

Imbeni, malaika,
Sifa za Yesu Bwana;
Pweke limetukuka
Jina lake Yesu.

Hatufai kuwa hai,
Wala hatutumai,
Ila kweli yeye ndiye
Atupumzishaye.

Dhambi pia na hatia
Ametuchukulia;
Twendeni na amani
Hata kwake Mbinguni.

Huliona tamu jina
La Yesu Kristo Bwana,
Yuna sifa mwenye kufa
Asishindwe na kufa.

Kila mume asimame,
Sifa zake zivume;
Wanawake na washike
Kusifu jina lake.

Na vijana wote tena,
Wapendao sana
Waje kwake wawe wake
Kwa utumishi wake.


Tazama Tenzi za Rohoni 1–164


Omba App ya Tenzi za Rohoni kwa Android

banner
Scroll to Top