Orodha kamili ya kozi za Diploma zenye mkopo wa HESLB2

          Kozi za Diploma Zenye Mkopo wa HESLB 2025/2026 | Mwongozo Kamili      
 

Kozi za Diploma Zenye Mkopo wa HESLB: Mwongozo Kamili 2025/2026

 

Jua orodha kamili ya programu zinazofadhiliwa, sifa za mwombaji, viwango vya fedha na jinsi ya kuomba mkopo wako kupitia mfumo wa OLAMS.

 

    Je, unasomea Diploma (Stashahada) na unajua kwamba unaweza kupata mkopo wa elimu kutoka Serikalini?     Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu (HESLB) inatoa mkopo kwa wanafunzi wa ngazi ya     Stashahada (Diploma/NTA Level 4–6) wanaosomea programu zilizopo kwenye vipaumbele vya Taifa.     Makala hii inakupa habari zote ulizohitaji — kutoka sifa, orodha ya kozi zinazofadhiliwa, hadi viwango     halisi vya fedha unazoweza kupata.  

 
    Mwanafunzi wa Diploma akisoma Tanzania — Mikopo ya HESLB  
   

HESLB na Mikopo ya Stashahada ni Nini?

 

    HESLB (Higher Education Students’ Loans Board) ni chombo cha Serikali cha Tanzania     kinachosimamia utoaji wa mikopo kwa wanafunzi wa elimu ya juu na ngazi ya kati. Kwa wanafunzi wa     Diploma/Stashahada, Bodi hutoa mkopo wa kugharamia ada, chakula, vitabu na mahitaji     mengine ya masomo — kwa masharti nafuu ya urejeshaji baada ya kuhitimu.  

 

    Mkopo huu hauna riba kama mikopo ya benki ya kawaida. Unarejeshwa kwa makato ya asilimia 15%     ya mshahara wako wa kila mwezi ukishaanza kufanya kazi, au kiwango kisichopungua     TZS 100,000 kwa mwezi kwa wale wanaojiajiri.  

   

Sifa Stahiki za Mwombaji Mkopo (Vigezo vya Msingi)

 

Ili uweze kufaidika na mkopo huu, lazima ukidhi masharti yafuatayo yaliyowekwa na HESLB:

 
    Zingatia: Ni lazima ukidhi     vigezo vyote vya msingi ndio uweze kuhitimu kupata mkopo. Kukosa kigezo kimoja     kunaweza kukuondoa kwenye orodha ya wanaostahili.  
 
       
  1. Uraia: Awe Mtanzania mwenye umri usiozidi miaka 27 wakati wa kuomba mkopo.
  2.    
  3. Udahili: Awe amedahiliwa rasmi katika taasisi ya elimu inayotoa elimu ya ngazi ya kati (Diploma/NTA) inayotambulika nchini.
  4.    
  5. Mfumo wa OLAMS: Awe amekamilisha na kuwasilisha maombi ya mkopo kupitia Mfumo wa Maombi ya Mkopo (OLAMS) — maombi ya karatasi hayakubaliwi.
  6.    
  7. Hana Ajira: Asiwe na ajira au mkataba wa kazi wa Serikali au sekta binafsi unaompatia mshahara au kipato chochote.
  8.    
  9. Ufaulu wa Kidato cha Nne (au zaidi): Awe amehitimu CSEE, Cheti (Astashahada), au ACSEE — ndani ya miaka mitano (2019 hadi 2023).
  10.  
 

Hali ya Kijamii na Kiuchumi (Zinazoongeza Kipaumbele)

 

Waombaji wenye hali zifuatazo hupewa kipaumbele zaidi katika upangaji wa mikopo:

 
       
  • Uyatima: Aliyefiwa na mzazi mmoja au wazazi wote wawili.
  •    
  • Kaya Duni (TASAF): Familia inayofadhiliwa na Mfuko wa Maendeleo ya Jamii (TASAF) au taasisi nyingine za kitaifa zinazotoa ufadhili kwa kaya zenye vipato duni.
  •    
  • Ulemavu: Mwombaji mwenye ulemavu wa mwili, au mzazi/mlezi wake mwenye ulemavu.
  •  
   

Maeneo 6 ya Kipaumbele ya Taifa — Kozi Zinazopata Mkopo

 

    HESLB haitoi mkopo kwa kozi zote. Mkopo unatoa kwa programu zinazoangukia kwenye     maeneo sita (6) ya kipaumbele yaliyoidhinishwa na Serikali kupitia Tangazo Namba     715 la tarehe 29 Septemba 2023. Maeneo hayo ni:  

 
    Afya & Sayansi Shirikishi     Elimu ya Ualimu     Usafiri & Usafirishaji     Uhandisi wa Nishati     Madini & Sayansi ya Ardhi     Kilimo & Mifugo  
 

Jedwali lifuatalo linaonyesha orodha kamili ya programu 26 zinazofadhiliwa katika kila eneo:

   
                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                       
#Eneo la KipaumbeleProgramu / Kozi ya DiplomaKifungu
1                         Afya na Sayansi Shirikishi
            (Health & Allied Sciences)          
Clinical Dentistry6.2.1
2Diagnostic Radiography
3Occupational Therapy
4Physiotherapy
5Clinical Optometry
6Dental Laboratory Technology
7Orthotics & Prosthetics
8Health Record & Information
9Electrical and Biomedical Engineering
10                         Elimu ya Ualimu
            (Education & Teaching)          
Stashahada ya Ualimu wa Sayansi (Fizikia, Kemia, Hisabati)6.2.2
11Stashahada za Elimu na Mafunzo ya Ufundi Stadi (TE&VET)
12                         Usafiri na Usafirishaji
            (Transport & Logistics)          
Aircraft Mechanics6.2.3
13Ship Building and Repair
14Railway Construction and Maintenance
15Global Logistics and Supply Chain Management
16                         Uhandisi wa Nishati
            (Energy Engineering)          
Renewable Energy Engineering (Hydro, Wind, Solar)6.2.4
17Pipeline, Oil and Gas Engineering
18                         Madini na Sayansi ya Ardhi
            (Mining & Earth Science)          
Lapidary and Jewelry6.2.5
19Mineral Processing
20                         Kilimo na Mifugo
            (Agriculture & Livestock)          
Leather Technology6.2.6
21Food Technology and Human Nutrition
22Sugar Production Technology
23Veterinary Laboratory Technology
24Horticulture
25Irrigation Engineering
26Agro Mechanization
 
 
    Kumbusho Muhimu: Kama kozi yako haipo kwenye     orodha hii ya programu 26, basi haustahili mkopo wa HESLB kwa ngazi ya Stashahada.     Unashauriwa kuchagua kozi zilizopo kwenye orodha hii wakati wa udahili ili uweze kufaidika na mkopo.  
   

Vyuo, Kozi na Vigezo vya Udahili (Kutoka NACTVET Guidebook 2025/2026)

 

    Ili kurahisisha mchakato wako, hapa kuna mifano ya vyuo mbalimbali na vigezo vya msingi vya udahili kwa baadhi ya kozi za afya kwa mujibu wa mwongozo rasmi wa NACTVET 2025/2026 uliotolewa:  

 
                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                               
Jina la Chuo (Mfano)Programu / Kozi (Diploma)Vigezo vya Udahili (O-Level)Muda
ACCRA College of Health and Allied Sciences
(Au Taasisi Nyingine)
Ordinary Diploma in Clinical MedicineUfaulu (Passes) usiopungua wa masomo 4 yasiyo ya dini ikiwemo Kemia, Biolojia na Fizikia/Sayansi ya Uhandisi. Ufaulu wa Hisabati na Kiingereza ni sifa ya ziada.Miaka 3
Taasisi Zilizoidhinishwa na NACTVETOrdinary Diploma in OptometryUfaulu (Passes) usiopungua 5 wa masomo yasiyo ya dini ikiwemo Biolojia, Kemia, Hisabati, Fizikia/Sayansi ya Uhandisi na Kiingereza.Miaka 3
Taasisi Zilizoidhinishwa na NACTVETOrdinary Diploma in Pharmaceutical SciencesUfaulu (Passes) usiopungua wa masomo 4 yasiyo ya dini ikiwemo Kemia na Biolojia. Ufaulu wa Hisabati na Kiingereza ni sifa ya ziada.Miaka 3
Taasisi Zilizoidhinishwa na NACTVETOrdinary Diploma in Public Health and Disaster ManagementUfaulu (Passes) usiopungua wa masomo 4 yasiyo ya dini ikiwemo Jiografia na Biolojia (au NVA Level III yenye cheti cha CSEE).Miaka 3
Zawadi Memorial Health Training Institute (Moshi)Ordinary Diploma in Nursing and MidwiferyUfaulu (Passes) usiopungua wa masomo 4 yasiyo ya dini ikiwemo Kemia, Biolojia na Fizikia/Sayansi ya Uhandisi. Ufaulu wa Hisabati na Kiingereza ni sifa ya ziada.Miaka 3
 
   

Viwango vya Fedha za Mkopo (Breakdown ya Kila Kipengele)

 

    Mkopo wa HESLB kwa ngazi ya Stashahada umegawanywa katika vipengele sita (6).     Kila kipengele kina kiwango chake cha juu. Hizi hapa chini ni kiwango cha juu (ceiling) —     si lazima upate kiwango chote, inategemea tathmini ya hali yako na chuo unachosomea.  

 
   
           
Chakula & Malazi
     
TZS 7,500
     
kwa siku (chuoni)
   
   
           
Ada ya Mafunzo
     
TZS 1,400,000
     
kwa mwaka (kwa chuo)
   
   
           
Vitabu & Viandikwa
     
TZS 200,000
     
kwa mwaka (kwa mwanafunzi)
   
   
           
Mahitaji ya Kitivo
     
TZS 300,000
     
kwa mwaka (kwa chuo)
   
   
           
Mafunzo kwa Vitendo
     
TZS 7,500
     
kwa siku (hadi siku 56/mwaka)
   
   
           
Gharama za Utafiti
     
TZS 100,000
     
kwa mwaka (baadhi ya programu)
   
 
   
                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                       
Kipengele cha MkopoKiwango cha JuuMpokeaji wa MalipoMaelezo Mafupi
Chakula na MalaziTZS 7,500 / sikuMwanafunzi moja kwa mojaKulingana na idadi ya siku za kalenda ya chuo
Ada ya MafunzoTZS 1,400,000 / mwakaChuo husika moja kwa mojaKulingana na ada halisi ya chuo husika
Vitabu na ViandikwaTZS 200,000 / mwakaMwanafunzi moja kwa mojaKwa ununuzi wa vitabu na vifaa vya masomo
Mahitaji Maalumu ya KitivoTZS 300,000 / mwakaChuo husika moja kwa mojaVifaa maalum vya kitivo (kwa programu zinazohitaji)
Mafunzo kwa VitendoTZS 7,500 / siku (max siku 56)Mwanafunzi moja kwa mojaKwa kipindi cha mafunzo ya vitendo (Clinical/Field)
Gharama za UtafitiTZS 100,000 / mwakaMwanafunziKwa baadhi ya programu zenye mradi wa utafiti
 
   

Nyaraka Zinazohitajika Wakati wa Kuomba Mkopo

 

    Wakati unawasilisha maombi ya mkopo kupitia OLAMS, utahitaji kuambatisha nyaraka     zifuatazo (kulingana na hali yako):  

 
       
  • Cheti cha Kuzaliwa: Kutoka RITA (namba ya uhakiki) kwa waombaji wa Tanzania Bara, au ZCSRA kwa waombaji wa Zanzibar.
  •    
  • Vyeti vya Vifo vya Wazazi (kwa Yatima): Kutoka RITA au ZCSRA ili kuthibitisha uyatima.
  •    
  • Fomu ya Ulemavu wa Mwombaji: Iliyoidhinishwa na Mganga Mkuu wa Wilaya (DMO) au Mganga Mkuu wa Mkoa (RMO).
  •    
  • Fomu ya Ulemavu wa Mzazi: Iliyoidhinishwa na DMO au RMO, ikiwa mzazi/mlezi ndiye mwenye ulemavu.
  •    
  • Namba ya Kaya ya TASAF: Kwa waombaji wanaotoka kwenye kaya zinazofadhiliwa na Mfuko wa Maendeleo ya Jamii (TASAF).
  •  
 
    Mdhamini: Mwombaji lazima aambatanishe     picha ya pasipoti ya mdhamini wake pamoja na nakala ya kitambulisho — Kitambulisho cha     Taifa (NIDA), Kadi ya Mpiga Kura, Leseni ya Udereva, Paspoti, au Kitambulisho cha Mzanzibari Mkaazi.  
   

Jinsi ya Kuomba Mkopo — Hatua kwa Hatua

 

    Mchakato wote wa kuomba mkopo unafanyika mtandaoni kupitia mfumo wa OLAMS     (Online Loans Application and Management System). Kumbuka kutumia namba ile ile ya     Mtihani wa Kidato cha Nne iliyotumika wakati wa udahili chuoni.  

 
       
  1. Tembelea tovuti: Nenda kwenye https://olas.heslb.go.tz na fungua akaunti yako ya SIPA.
  2.    
  3. Jaza Fomu: Jaza fomu ya maombi kwa ukamilifu na usahihi. Hakikisha taarifa za benki (kama unazo) na Namba ya NIDA zimewekwa vizuri.
  4.    
  5. Lipia Ada ya Maombi: Lipia TZS 30,000 kupitia benki (NMB, CRDB, TCB, NBC) au mitandao ya simu (M-Pesa, TigoPesa/EzyPesa, Airtel Money, HaloPesa, AzamPesa, T-Pesa).
  6.    
  7. Pakua na Saini Fomu: Baada ya kukamilisha mtandaoni, pakua fomu, igonge muhuri sehemu husika, isaiini, na kuambatisha nyaraka zote.
  8.    
  9. Wasilisha Fomu: Rudisha kurasa zilizosainiwa (kurasa 2 na 5) ya fomu ya maombi katika mfumo wa OLAMS.
  10.    
  11. Angalia Matokeo: Orodha ya watakaopangiwa mikopo itatangazwa kwenye akaunti yako ya SIPA au kwenye tovuti ya HESLB: www.heslb.go.tz.
  12.  
   

Masharti ya Urejeshaji wa Mkopo

 

    Mkopo wa HESLB si zawadi — ni mkopo wa kweli unaolazimika kurejeshwa baada ya kuhitimu.     Hata hivyo, masharti ni mazuri sana ukilinganisha na mikopo ya benki ya kawaida:  

 
       
  • Wafanyakazi (Sekta Rasmi): Makato ya asilimia 15% (15%) ya mshahara wako wa kila mwezi.
  •    
  • Wajasiriamali (Sekta Isiyo Rasmi): Kiwango kisichopungua TZS 100,000 kwa mwezi.
  •    
  • Ada ya Uendeshaji: Mkopo wote unatozwa asilimia moja (1%) ya deni la msingi kwa mara moja tu.
  •    
  • Kuacha Masomo: Ikiwa utaacha au kukatishwa masomo, mkopo wote utalipwa kwa mkupuo.
  •  
   
   

      Hitimisho — Tumia Fursa Hii Vizuri!    

   

      Serikali ya Tanzania kupitia HESLB imeweka mfumo mzuri wa kuhakikisha wanafunzi wa Stashahada       wanaosomea programu za kipaumbele wanapata fedha za kutosha. Kama unasomea kozi yoyote kati ya       26 zilizoorodheshwa katika maeneo sita ya kipaumbele,       usikose kuomba mkopo wako kupitia OLAMS.       Kumbuka: fedha za HESLB zinakwenda moja kwa moja kwenye akaunti yako na kwa chuo chako —       usalama na uwazi ni vipaumbele vyao.    

 
   
   
     

Pata Ushauri wa Kuchagua Kozi, Notes na Past Papers

     

        Unahitaji mwongozo wa kuchagua kozi bora inayostahili mkopo? Au unahitaji         notes za masomo ya afya, maswali na mitihani ya zamani?         Wasiliana nasi tukusaidie.      

     

Pia tunatoa huduma za Admission (Udahili), Research, na vifaa vya kujifunzia.

     

Tuma ujumbe wa WhatsApp sasa hivi upate msaada haraka!

         
 
  2026 Devine Vision Tech | Huduma za Kitaalamu kwa Wanafunzi wa Afya
Scroll to Top