Diploma ya Physiotherapy
Jifunze jinsi ya kuwa mtaalamu wa Tiba ya Viungo, soko la ajira, na vyuo vinavyotoa kozi hii Tanzania.
Hivi unajua kwamba unaweza kuwa mtaalamu wa afya na kuwasaidia wagonjwa kupona bila kutegemea vidonge na sindano pekee? Ndiyo, inawezekana kabisa. Leo nakusogeza karibu na kozi ya Diploma ya Physiotherapy, au kwa Kiswahili rahisi zaidi tunaita Tiba ya Viungo.
Hii ni kozi adimu sana hapa Tanzania, lakini kwa upande mwingine ina soko kubwa la ajira pamoja na fursa nzuri za kujiajiri.
Kama wewe ni mwanafunzi, mzazi, au mtu yeyote unayetafuta mwelekeo mpya wa taaluma, basi karibu nikueleze kwa kina kozi hii inahusu nini, utasoma masomo gani, na nitakupa orodha kamili ya vyuo vyote vya Serikali na Binafsi vinavyotoa kozi hii hapa nchini.
Physiotherapy ni Nini?
Kwa lugha nyepesi kabisa, Physiotherapy ni taaluma ya kurejesha uwezo wa mwili kufanya kazi kama kawaida.
Mfano wa wagonjwa wanaohudumiwa:
- Mtu aliyepata ajali na kuvunjika mifupa.
- Mzee aliyepata kiharusi (stroke) na kushindwa kutembea.
- Mtu mwenye maumivu makali ya mgongo, shingo au viungo.
Watu hawa hawahitaji dawa za maumivu pekee. Wanahitaji mtaalamu wa viungo atakayemsaidia mwili wao kurudi katika hali ya kawaida kwa kutumia:
- Mazoezi tiba (Therapeutic exercises).
- Misaji ya kitaalamu (Physiotherapy massage).
- Matumizi ya vifaa maalum vya tiba (kama Ultrasound na TENS).
Utasoma Nini Katika Kozi Hii?
Kozi ya Diploma ya Physiotherapy huchukua miaka mitatu (3), na ndani ya muda huo utajifunza mambo muhimu sana, hasa katika maeneo makuu matatu:
- Anatomia: Hapa utajifunza ramani ya mwili wa binadamu: mifupa, misuli, mishipa, na viungo vilipo na jinsi vinavyofanya kazi.
- Ukarabati (Rehabilitation): Utajifunza mbinu za kitaalamu za kumsaidia mtu kusimama tena, kutembea, na kutumia mikono au miguu baada ya kuumia au kuugua.
- Matumizi ya vifaa vya kisasa: Utajifunza kutumia mashine na vifaa vinavyosaidia wagonjwa kupona kwa haraka na usalama.
Sifa za Kujiunga
Sifa za kujiunga na kozi hii si ngumu, lakini lazima uwe na msingi wa sayansi:
- Awe na Cheti cha Kidato cha Nne.
- Awe na ufaulu wa angalau alama “D” nne.
- Awe amesoma na kufaulu masomo ya Sayansi, yaani: Biology, Chemistry na Physics.
Haya ni muhimu kwa sababu kozi hii inahusiana moja kwa moja na mwili wa binadamu na sayansi ya afya.
Fursa za Ajira na Kujiajiri
Baada ya kumaliza kozi ya Physiotherapy (Tiba ya Viungo), unapata fursa nyingi za kazi na biashara:
- Hospitalini: Kuajiriwa hospitali za Serikali au Binafsi.
- Rehabilitation Centres: Kufanya kazi vituo vya urekebishaji wagonjwa wa ajali na ulemavu.
- Huduma za Nyumbani (Home Care): Kuhudumia wazee na wagonjwa majumbani.
- Michezoni: Kuwa Physiotherapist wa timu za mpira au wanamichezo.
- Kujiajiri: Kufungua kliniki yako binafsi ya mazoezi na tiba.
Vyuo Vinavyotoa Kozi Hii Tanzania
Sasa twende kwenye swali muhimu zaidi: utasoma wapi? Hii hapa ni orodha kamili ya vyuo vilivyosajiliwa:
1. Vyuo vya Serikali
- Kilimanjaro College of Health and Allied Sciences – Moshi
- Mbeya College of Health and Allied Sciences – Mbeya Jiji
- Mwanza College of Health and Allied Sciences – Nyamagana, Mwanza
2. Vyuo vya Mashirika ya Dini (FBO)
- Kolandoto College of Health Sciences – Shinyanga
- Machame Health Training Institute – Hai, Kilimanjaro
3. Vyuo vya Binafsi (Private)
Dar es Salaam:
- City Institute of Health and Allied Sciences – Ilala
- Kigamboni City College of Health and Allied Sciences – Kigamboni
- City College of Health and Allied Sciences – Temeke
- Taifa Institute of Health and Allied Sciences – Kinondoni
- Vignan Institute of Science and Technology – Kinondoni
Mwanza:
- City College of Health and Allied Sciences – Nyamagana
- Sir Edward College of Health and Allied Sciences – Nyamagana
Mikoa Mingine:
- Kilimanjaro Institute of Health Sciences – Arusha Jiji
- Mgao Health Training Institute – Njombe
- Mkuranga College of Health and Allied Sciences – Pwani
- Mlimba Institute of Health and Allied Sciences – Kilombero, Morogoro
Unahitaji Msaada Zaidi?
Je, unatafuta Notes za masomo, Maswali na Majibu (Past Papers) au unahitaji ushauri wa kimasomo? Pia tunatoa huduma za kuandika Research na Ripoti mbalimbali.
