Ratiba ya Chanjo za Kuku wa Kienyeji
Mwongozo rahisi wa kukuza kuku wenye afya, uzito, na kuepuka vifo vya vifaranga. Pata ratiba ya Mdondo, Gumboro na Ndui.
Je, unatafuta ratiba sahihi ya chanjo za kuku ili kuepuka hasara? Ufugaji wa kuku wa kienyeji unalipa sana ikiwa utazingatia kanuni bora za afya. Changamoto kubwa inayowarudisha nyuma wafugaji wengi Tanzania ni vifo vya vifaranga vinavyosababishwa na magonjwa kama Mdondo (New Castle) na Ndui.
Hapa chini tumekuandalia jedwali kamili la dawa na chanjo kuanzia siku ya kwanza hadi kuku anapoanza kutaga.
Jedwali la Ratiba ya Chanjo na Dawa
| Umri (Siku/Wiki) | Ugonjwa / Tatizo | Dawa / Chanjo | Njia ya Utoaji |
|---|---|---|---|
| Siku 1 – 3 | Kusafisha Tumbo & Stress | Vitamini & Glucose | Maji ya Kunywa |
| Siku 3 – 5 | Kuzuia Vifo vya Mapema | Antibiotiki (Chick Formula) | Maji ya Kunywa |
| Siku ya 7 | Mdondo (New Castle) | Hitchner B1 | Tone 1 jichoni/pua |
| Siku ya 14 | Gumboro (IBD) | Gumboro Intermediate | Maji ya Kunywa |
| Siku ya 21 | Mdondo (Marudio) | La Sota | Maji ya Kunywa |
| Siku ya 28 | Gumboro (Marudio) | Gumboro Booster | Maji ya Kunywa |
| Wiki ya 6 – 8 | Ndui ya Kuku (Fowl Pox) | Fowl Pox Vaccine | Kuchanja kwenye bawa |
| Wiki ya 9 | Minyoo | Dawa ya Minyoo | Maji ya Kunywa |
| Kila Miezi 3 | Mdondo (Kinga Endelevu) | La Sota / I-2 | Maji ya Kunywa |
Mambo Muhimu ya Kuzingatia
- Usichanje Kuku Mgonjwa: Chanjo hutolewa kwa kuku mwenye afya tu. Ukichanja mgonjwa, unaharakisha kifo chake.
- Maji Safi: Hakikisha maji unayotumia kuchanganya chanjo hayana klorini (Chlorine). Tumia maji ya kisima au mvua.
- Muda Sahihi: Toa chanjo asubuhi na mapema au jioni wakati wa baridi. Jua kali linaua nguvu ya chanjo.
- Vitamini: Baada ya kutoa chanjo (kesho yake), wape kuku vitamini (Multivitamins) ili kupunguza stress.
Magonjwa Hatari kwa Kuku wa Kienyeji
1. Mdondo (New Castle)
Huu ndio ugonjwa unaoua kuku wengi zaidi Tanzania. Kuku hupinda shingo, kuharisha kijani, na hufa kwa wingi ghafla. Tiba: Hakuna tiba, kinga pekee ni chanjo ya Hitchner B1 na Lasota kwa wakati sahihi.
2. Ndui (Fowl Pox)
Kuku hutokea vipele sehemu zisizo na manyoya (macho, mdomo, upanga). Husababisha upofu na kushindwa kula. Kinga: Chanjo ya Ndui wiki ya 6-8.
Maswali Yanayoulizwa Mara kwa Mara (FAQs)
Je, Unahitaji Ushauri wa Ufugaji?
Ufugaji wa kuku unahitaji maarifa sahihi. Kama unahitaji msaada wa kupata vifaranga bora, vyakula vya kuku, au ushauri wa kitaalamu kuhusu magonjwa, tupigie simu sasa.
Fika ofisini kwetu DeVine Vision Tech iliyopo Kisesa, Mwanza.
