Ordinary Diploma in Community Development
(Stashahada ya Maendeleo ya Jamii)
Kuwa chachu ya mabadiliko. Jifunze kusimamia miradi, kuhamasisha jamii, na kuleta maendeleo endelevu.
Community Development (Maendeleo ya Jamii) ni kozi inayolenga kuwawezesha wananchi kujiletea maendeleo wenyewe. Tofauti na Social Work (inayotatua matatizo ya mtu mmoja mmoja), Community Development inatazama jamii kwa ujumla—kujenga shule, zahanati, vikundi vya ujasiriamali, na miradi ya maji.
1. Sifa za Kujiunga (Admission Requirements)
Ili kujiunga na kozi hii kwa mwaka wa masomo 2025/2026, mwombaji lazima akidhi moja ya vigezo vifuatavyo:
- Awe na Cheti cha Kidato cha Nne (CSEE).
- Awe na ufaulu wa Alama “D” Nne (4) au zaidi.
- Masomo hayo lazima yawe yasiyo ya dini (Non-religious subjects).
- Ufaulu wa somo lolote (Sanaa au Sayansi) unakubalika.
- Awe na Basic Technician Certificate (NTA Level 4) katika mojawapo ya fani hizi:
- Community Development (Maendeleo ya Jamii)
- Social Work (Ustawi wa Jamii)
- Gender (Jinsia)
- Youth Work (Kazi za Vijana)
- Awe na Cheti cha Kidato cha Sita (ACSEE).
- Awe na angalau Principal Pass Moja (1) na Subsidiary Pass Moja (1) katika masomo makuu (Principal Subjects).
2. Utajifunza Nini? (Umuhimu wa Kozi)
Kozi hii inakuandaa kuwa kiongozi na mhamasishaji. Utajifunza:
3. Fursa za Ajira na Kujiendeleza
Wahitimu wa Community Development wanaajirika kirahisi serikalini na sekta binafsi:
Afisa Maendeleo ya Jamii (CDO)
Kuajiriwa na Halmashauri za Wilaya/Miji kufanya kazi kata kwa kata, kusimamia mikopo ya asilimia 10 (Wanawake, Vijana, Wenye Ulemavu).
Mashirika ya Kimataifa (NGOs)
Kufanya kazi kama Mratibu wa Miradi (Project Coordinator) katika taasisi kama World Vision, Plan International, na nyinginezo.
Mashirika ya Kijamii (CBOs)
Kusimamia taasisi za kijamii zinazotoa huduma za maji, elimu, au afya vijijini.
Unahitaji Msaada wa Kujiunga?
Je, unatafuta chuo bora cha Community Development? Au unahitaji msaada wa kufanya maombi (Online Application)?
Sisi DeVine Vision Tech tunakusaidia kuchagua vyuo na kufanya maombi kwa umakini mkubwa.
Fika ofisini kwetu: Kisesa, Mwanza.
